Niki wa Pili : Sina cha kukumbuka kwa Obama


Rais wa Marekani anayemaliza muda wake Barack Obama.

Rapa Niki wa Pili amefunguka na kusema yeye hana cha kukumbuka kwa Rais wa Marekani Barack Obama ambaye tarehe 20 mwezi huu anamaliza muda wake kuitumikia Marekani kama Rais 44 na kukabidhi ofisi kwa Rais Mteule wa Marekani Donald Trump.

Niki wa Pili aliweka wazi sababu kubwa inayomfanya asiwe na cha kukumbuka kutoka kwa Rais Barack Obama kwanza ni kutokana na Rais kutokuwa na utu na serikali yake kushiriki katika mauaji ya watu na kukatisha haki za watu kuishi katika baadhi ya maeneo.

"Mimi kwangu sina cha kumkumba Obama kwa sababu mimi kwanza ni mtu naye amini katika utu na naamini kila binadamu ana haki ya kuishi hivyo nikimkumbuka Obama namkumbuka madrone yamedondoshwa huko na kuuwa watu wasio na hatia zaidi ya elfu saba, ukienda Afghanistan amesambaratisha taifa la Iraq ukiangalia Libya.

Kutokana na kitendo hicho Niki wa Pili anasema yeye kama mfuasi wa utu hawezi kumkumbuka Barack Obama na wala hawezi kumuunga mkono.

"Mimi kama mfuasi wa utu niko against na mtu yoyote anayekandamiza utu sehemu yoyote duniani.

Hivyo siwezi kumuunga mkono Obama sababu mimi namuona hakuwa mfuasi wa utu kwa hiyo mimi si mtu wangu kabisa" alisema Niki Wa Pili

No comments

Content by MwasebaINFO.All RIghts Reserved. Powered by Blogger.