Watu 4 wauawa na 5 kujeruhiwa kwa kupigwa risasi Arumeru.

Watu wanne wakazi wa kijiji cha Kandaskiriet kata ya Oldonyosambu wilayani  Arumeru wameuawa na wengine watano kujeruhiwa vibaya baada ya kupigwa risasi na askari wa SUMA JKT ambao ni walinzi wa shamba la miti la serikali la Meru USA Plant.

Akithibitisha kutokea kwa mauaji hayo Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo amesema tukio hilo limetokea Januari ishirini na nne wakati askari hao wakiendelea na operesheni ya kuondoa mifugo iliyoingia ndani ya shamba hilo na ndipo walipokutana na kundi la wananchi wakiwa na silaha mbalimbali za jadi ambao waliwashambulia na wao wakalazimika kujibu mashambulizi hayo.

Wakizungumza hospitalini Mount Meru walipolazwa majeruhi na miili ya marehemu kuhifadhiwa,baadhi ya majeruhi akiwemo William Kilangwa,Mathayo Masharubu na Thobias Lazaro.

Kwa upande wake diwani wa kata ya Oldonyosambu Raymond Leirumbe akaliomba Jeshi la polisi kuharakisha upelelezi wa tukio  hilo mapema ili kuwaridhisha wananchi ambao kwa sasa wako kwenye taharuki kubwa ombi ambalo Kamanda Mkumbo anaahidi kulifanyia kazi haraka akiwataka wananchi hao kuwa na subira.

No comments

Content by MwasebaINFO.All RIghts Reserved. Powered by Blogger.