Taarifa ya Kutokea Kwa Hitilafu Katika Grid ya Taifa

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linawataarifu Wateja wake na Umma kwa ujumla kuwa kumetokea hitilafu katika Kituo kikubwa cha kupoza na kusambaza Umeme cha Ubungo, hitilafu hiyo imesababisha Grid ya Taifa kutoka na kusababisha Mikoa yote iliyounganishwa katika Grid ya Taifa kukosa Umeme.

Mafundi wanaendelea na jitihada ya kurejesha Umeme katika hali yake ya kawaida.

Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu wowote unaojitokeza.

Imetolewa na; Ofisi ya Uhusiano

TANESCO Makao Makuu

No comments

Content by MwasebaINFO.All RIghts Reserved. Powered by Blogger.