Breaking News:Mbunge wa Kilombero Morogoro (CHADEMA ) ahukumiwa miezi 6 jela Bila Faini

Mbunge wa Jimbo la Kilombero, Peter Lijualikali na Dereva wake, John Kibasa wamehukumiwa kwenda jela miezi sita bila faini kwa kosa la kufanya vurugu kipindi cha uchaguzi mwaka 2015.

Hukumu hiyo imetolewa leo katika Mahakama ya Wilaya ya Kilombero na sasa amepelekwa gerezani huku taratibu za kukata rufaa zikiendelea.

Hukumu hiyo ilisomwa chemba lakini wabunge wawili wa Chadema Joseph Haule (Mikumi) na Ester Bulaya (Bunda Mjini) waliingia na kusikiliza hukumu.


No comments

Content by MwasebaINFO.All RIghts Reserved. Powered by Blogger.