Tumdai Ben Saanane Mpaka Apatikane

Kelele nyingi kuhusu Makonda na umaarufu wa jina la Daud Bashite uliopo sasa, umenifanya nione kuwa kumbe Watanzania wakiwa na mshikamano na kuhoji jambo linawezekana.

Kelele za mitandaoni kuhusu Makonda kama zingetumika kuhoji mahali alipo Ben, zingef APATIKANE

Kelele nyingi kuhusu Makonda na umaarufu wa jina la Daud Bashite uliopo sasa, umenifanya nione kuwa kumbe Watanzania wakiwa na mshikamano na kuhoji jambo linawezekana.

Kelele za mitandaoni kuhusu Makonda kama zingetumika kuhoji mahali alipo Ben, zingefanya mamlaka za nchi zijue kuwa suala la Ben lina athari kubwa kijamii na halipaswi kufanyiwa mzaha au kupuuzwa.

Mwezi wa nne sasa Ben hajulikani alipo. Inatakiwa watu wapaze sauti na Serikali itambue kuwa siyo rahisi Watanzania wapotelewe na ndugu yao kisha wanyamaze kama hakijatokea kitu.

Naamini kuwa Serikali ikiamua kulivalia njuga suala la Ben, majibu yatapatikana na itajulikana ni wapi alipotelea. Ben hapaswi kupotea kama Mtanzania wa enzi za ujima. Ben ni kijana wa kisasa, akifuatiliwa zipo alama alizoacha zitatoa majibu.

Niliwahi kuandika kuwa Tanzania siyo Alaska, Marekani, ambako watu mamia hupotea kila mwaka pasipo kujulikana walipokwenda. Tanzania ni Tanzania, mtu akipotea tunajua kuna chanzo. Hicho chanzo ndiyo tukitafute na tukijue.

Hivyo basi, kila Mtanzania anapaswa kuhakikisha anaifanya Tanzania yake inakuwa si rahisi kwa matukio ya hovyo, ama kupoteza watu au watu kujipoteza. Watanzania wanatakiwa kuwa na mshikamano wa kuhoji kuhusu Ben na majibu yenye kutosheleza yatolewe.

Zingatia kuwa kama Ben amepotezwa, waliocheza mchezo huo wataendelea kucheza na wengine, ipo siku watakuja kwako au kwa ndugu yako. Ndiyo maana nimesema Watanzania wanatakiwa kuhoji sana ili kama wapo watu hao, wapate ujumbe kuwa Tanzania siyo rahisi.

Hata kama ni Ben mwenyewe alijipoteza, naye apate ujumbe kuwa Tanzania siyo rahisi. Kwamba huwezi kufanya mchezo wa hovyo kwa nchi yao kisha ukafanikiwa kwa urahisi tu. Tuendelee kuhoji Ben. Tumuombe Mungu amlinde Ben. Kama kuna watu wamecheza mchezo mchafu, basi Mungu atusaidie kuwabaini.

Ndimi Luqman MALOTO

No comments

Content by MwasebaINFO.All RIghts Reserved. Powered by Blogger.