ALIYO YASEMA MWAKYEMBE KUHUSU ALIPOFIKIA JUU YA UVAMIZI WA CLOUDS TV

March 29, 2017 Waziri wa Habari, utamaduni, sanaa na micheo Dr. Harrison Mwakyembe alifanya mkutano na Waandishi wa habari Dodoma na kuzungumzia mikakati ya Wizara yake.

Moja ya swali aliloulizwa na wanahabari ni kuhusu ripoti iliyoachwa na Waziri wa zamaniNape Nnauye kuhusu uchunguzi wa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makondakudaiwa kuvamia ofisi za Clouds Media huku akiwa na Asjari wenye silaha.

Wengi mnauliza nimeifanyia kazi gani ripoti ya Nape, mimi hiyo ripoti sijaiona na kama mwanasheria kwangu ni mwiko na sitapeleka taarifa ambayo haijakamilika’ -Waziri Mwakyembe

Kupitia vyombo vya habari taarifa imeeleza kuwa ushahidi ulitolewa na upande wa Clouds Media na mkakiri kuwa upande wa pili haukupatikana’ –Waziri Mwakyembe

Huwezi kuwa Hakimu kwenye suala lako wewe mwenyewe, kufanya hivyo ni ubatili kwahiyo hata mimi ningekuwa ni mwandishi wa habari ningesema hili jambo siliwezi kwakuwa linanihusu na mimi’ -Waziri Mwakyembe

Kanuni zinataka kusikiliza upande wa pili, sasa mmeshasema kitu kina upande mmoja alafu nimpelekee kiongozi wangu..NO, mimi kazi yangu ni kupata maelezo ya upande wa pili na nitapata’ –Waziri Mwakyembe

Hili jambo ni lakufa na kupona, yani niache kukutana na wakuu wa idara mbalimbali hapa kuhakikisha nakuza suala la sanaa na kuhakikisha vijana wetu hawaendelei kuibiwa nibaki kuhangaikia suala la ripoti’ -Waziri Mwakyembe

Mimi sikuapa kwa jambo hilo moja pekee lakini mimi ni mwanasheria mkongwe na nitahakikisha nalifuatilia lakini mimi sitaunda kamati katika jambo hilo’ –Waziri Mwakyembe

Lengo letu ni kuhakikisha hatutakuwa na matukio ya namna hiyo katika safari lakini tukitoka na kauli za papara tutakuwa tunajitafutia matatizo hapo mbeleni ’ -Waziri Mwakyembe

No comments

Content by MwasebaINFO.All RIghts Reserved. Powered by Blogger.