Video: Mzee Wa Upako Anthony Lusekelo aubiri kwa kutumia Muziki ya Darassa

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) Ubungo-Kibangu jijini Dar es salaam, Lusekelo Anthony ‘Mzee wa Upako’ ametrendi mtandaoni wiki hii baaada ya kusambaa kwa video inayomwonyesha akiwaubiria watumishi wa kanisa lake kwa kutumia wimbo ‘Muziki’ wa Darassa.

Mchungaji huyo amedai ameamua kubadilisha namna ya kuubiri kwa kuwa dunia inaenda kila siku ikibadilika.

“Lazima ujue huku duniani watu wanaongea nini, ukitoka hapo ndio utajua dunia inataka nini. Utajua kumbe ‘Kamatia Chini’ imefulia, iko acha maneno weka muziki,” alisema mchungaji huyo. “Mimi sio yule mchungaji wa kizamani, Acha maneno weka muziki,”

No comments

Content by MwasebaINFO.All RIghts Reserved. Powered by Blogger.